SAFARI YA MAFANIKIO.
(Picha;Sir Moris) Azimio langu la kujiunga na chuo kikuu wakati nilipokuwa chuo Cha upili hatimaye iliwadia.Baada na kunyakua alama za juu katika mtihani wa kitaifa wa shule ya upili, nilipata mwaliko katika chuo kikuu Cha kiufundi Cha Mombasa.Sikufikiria mara mbili mbali nilijitosa mzimamzima ili nikajishuhudie yote yatendekayo katika vyuo vikuu.Nilipokwisha kujisajili nilielekezwa katika darasa langu.Maisha niliyoyatarajia huku yalikuwa kinaya.Nilijifunza jinsi ya kujitegemea pasipo mzazi au mwalimu . Katika pilkapilka zangu za masomo,nilikuja kugundua Kuna watu wenye sampuli tofauti humu chuoni;wale wapole,wenye hasira,wale waraibu wa mihadarati na wanaozama katika Lindi la shinikizo la rika.Nilijitahidi sana nisiwe mwenye sifa mbaya kadri niwezavyo.Miaka ilizidi kusonga hadi ilipofika muda wa kiambatisho almaarufu field attachment.Huo ulikuwa muda wa wanafunzi kujiendeleza kimasomo katika kiwango Cha uhalisia almaarufu practicals.Kwa kuwa nilikuwa nasomea uanahabari na utengenezaji...